By
Monica Okwany
Mwanamke
mwenye umri wa 25 amepewa kifungo cha miaka mitatu baada ya kuiba mototo wa
miaka miwili.
Irene
Ayambuta alitekeleza wizi huo mnamo tarehe 18/9/2012 katika mtaa wa Oruba,
kaunti ya Migori.
Bi
Grace Wanyenyi Mutatiro alimwacha mwanawe Faith Wati akicheza na wenzake na
kwenda sokoni kulangua parachichi na aliporudi alimkuta mtoto wake hayupo.
Aliambiwa
na majirani kwamba mtoto wake alikuwa amechukuliwa na mwanamke ambaye
hawakumtambua. Alimtafuta mtoto wake hadi nchi jirani ya Tanzania.
Alipata
habari siku mbili baadaye kwamba mtoto wake alipatikana. Hapo ndipo wananchi
walimvamia Bi Irene na kumpiga na kumjeruhi vibaya.
Aliokolewa
na polisi ambao walimpeleka katika hospitali ya wilaya ya Migori kwa matibabu
kabla ya kupelekwa korokoroni.
Alikubali
mashtaka mbele ya hakimu mkaazi Bw. Edwin Nyaga ambaye alimpa kifungo cha miaka
mitatu.
©KNA,
Septemba 24, 2012