Wednesday, 3 October 2012

Baba aliyemnajisi bintiye wa miaka tisa atiwa kizuizini na polisi.

TAREHE 19 SEPTEMBA 2012

 NA MONICA OKWANY

Mwanamme wa umri wa makamo anazuiliwa katika kituo cha polisi huku uchunguzi ukiendelea kwa madai ya kumnajisi bintiye wa miaka tisa.

Bw Nicholas Abich alimnajisi bintiye mnamo tarehe 4/9/2012 wakati alikwenda kuchukua dawa aliyotumwa na mamake kutoka kwa nyumba.

Akithibitisha kisa hicho mkuu wa polisi mjini Migori Bw. Alfred Makoma alisema kwamba mwanaume huyo alimkamata bintiye na kumangusha kitandani mwao na kumfanyia kitendo hicho cha unyama.

“binti huyo alikimbia na kumweleza mamake ambaye alimjulisha chifu wa eneo la Rapon huko Awendo aliwaarifu polisi ambao walimtia mbaroni Nicholas” bw .Makoma alisema

Aidha bw. Makoma aliongeza kwamba visa kama hivi vimeongezeka sana katika maeneo ya migori akihoji kwamba uchunguzi unaendelea na iwapo mshukiwa atapatikana na hatia basi atachukuliwa hatua kali ya kisheria.

No comments:

Post a Comment