Wednesday, 3 October 2012

Mwanamme wa miaka 63 afikishwa mahakamani kwa kosa la wizi wa kimabavu

Na Monica Okwany

Mwanamme wa umri wa miaka 63 hivi leo amefikishwa mbele ya mahakama ya Migori akikabiliwa na kosa la wizi wa kimabavu.

James Leparan Naiyioma anadaiwa kuwa mnamo tarehe 16/1/2011 katika mtaa wa Ranen wilayani Migori, akishirikiana na wengine ambao hawakuwa mahakamani walikuwa wamejihami kwa silaha hatari zikiwemo bunduki, panga na rungu walimvamia Bw. Richard Kones Oyer na kumwibia mali yake ikiwemo nguo, redio aina ya sony, busta ya runinga, simu za rununu 12, ‘ airtime voucher’ yenye thamani ya shilingi 60 000 na pesa taslimu shilingi 227 000.

Hata hivyo Bw. Leparan alikanusha mashtaka hayo mbele ya hakimu mkaazi Bw Edwin. M. Nyaga.

Aliachiliwa kwa dhamana ya shilingi 100 000 na udhamini wa kiasi hicho.

Kesi hiyo itasikizwa tarehe 29/10/2012.

No comments:

Post a Comment