MONICA OKWANY
Tume huru ya uchaguzi na mipaka(IEBC) imeanza uhamasishaji wa umma kuhusiana na usajili wa wapiga kura kwa njia ya kielektroniki.
Afisa wa tume hiyo eneo bunge la Migori Bw. Mourice Raria, aliwasilisha
ramani mpya ya maeneo ya kupiga kura.
Aliwataka wapiga kura kufahamu na kuelewa kodi zinazotumika kuwasilisha
maeneo mapya na za awali ya kupiga kura katika kaunti ya Migori.
Alisema kwamba madhumuni ya mradi huo ni kuhakikisha kwamba ushirikiano
katika usajili wa wapiga kura umeimarishwa.
Bw. Mourice aliongeza kuwa uwekezaji wa umeme utaimarishwa
katika vituo vyote vya kupiga kura.
Akizungumza katika mkutano na wadau mjini Migori, Bw Mourice
aliwahakikishia wapiga kura kuwa makarani wataelimishwa ipasavyo na kwa wakati
huo huo hali ya usalama itaimarishwa katika vituo vyote vya upigaji kura kabla
na baada ya kupiga kura.
Tume huru ya uchaguzi na mipaka inanuia kuwasajili wapiga
kura 65000 katika maeneo bunge ya Suna Magharibi na Mashariki.
No comments:
Post a Comment