Tuesday, 2 October 2012

Mwanamme ashtakiwa kwa kumiliki bhangi ya shillingi laki mbili

Na Monica Okwany
Mwanamme aliye na umri wa miaka 21 amefungwa kwa kosa la kumiliki misokoto mitano ya bangi huku mwingine ashtakiwa kwa kulaghai mwenzake shilling 249,000.
Duncan Onyango Ochieng alifikishwa mbele ya hakimu mkaazi Bi Grace Kiruguma mnamo tarehe 10/09/2012 na kushtakiwa kwa kosa la kuhifadhi bangi yenye gramu 50 iliyo na thamani ya shilingi 50. kinyume cha sheria nambari 4 sehemu ya 3 ya mwaka wa1994 .
Akielezea mahakama, mkuu wa mashtaka Bw.G Kimani alisema kwamba mshukiwa alitiwa mbaroni na babake mzazi Bw. Ochieng Ouya aliyesaidiwa na wanakijiji baada ya kuteketeza nyumba yao katika kata ya Mapera kaunti ya Migori.
Mshukiwa ambaye ni mkulima katika kata ndogo ya Got Jope Abila, alishikwa na kufanyiwa msako na wanakijiji ambapo misokoto mitano ya bangi ilipatikana ndani ya mfuko wake wa suruali ndefu.
Mahakama ilimpata na hatia na kumpa kifungo cha mwaka mmoja.
Kwingineko katika mahakama hiyo mwanamme aliye na umri wa miaka 41 alifikishwa mbele ya hakimu mkaazi Bi Grace Kirugumi mnamo tarehe 10/09/2012 kwa kosa la kumlaghai Bw Rodgers Abisai shilingi 249 000 tarehe 2/06/2011 kwa madai ya kuteuliwa na kupewa mamalaka ya kuchunguza na kumiliki mali ya marehemu Bw. George Riogi Motende.
Mshukiwa ambaye alitambuliwa kama Bw. Robert Gideon Onderi alipatikana na hatia ya kuchukua pesa kwa njia ya ulaghai kinyume cha sheria.
Pia, alipatikana na hatia ya kutoa ushahidi wa uongo tarehe 2/7/2009 mbele ya hakimu Bw. Kibet Samba kwa kuapa kuwa alikuwa nduguye marehemu Bw.George Rioyi Molende ili kupata barua ya urithi wa mali ya marehemu.
Mshukiwa ambaye ni mkaazi wa mtaa wa Nyamesango wilaya ya Gucha mjini Kisii bado anazuiliwa huku uchunguzi ukiendelea.

No comments:

Post a Comment