Tuesday, 2 October 2012

Mwanamke wa miaka 36 kizuizini kwa kumdhulumu kimapenzi Kijana wa miaka 17

Na Monica Okwany

Mwanamke wa umri wa miaka 36 anazuiliwa katika kituo cha polisi cha Awendo kwa kosa la kumdhulumu kimapenzi mvululana wa miaka 17.

Carolyn Atieno alikamatwa mnamo tarehe nne mwezi wa tisa mwaka huu katika kijiji cha ominde akimdhulumu George oliech , mwanafunzi wa darasa la sita katika shule ya msingi ya Awendo.

Akithibitisha kisa hicho, mkuu wa polisi mjini Migori bw. Alfred Makoma alisema kwamba mshukiwa alifumaniwa akitekeleza kitendo hicho chumbani mwake.

Bw .makoma alisema mwanamke huyu alimwalika kijana huyu chumbani kwake kwa madai ya kumpa kikombe cha chai na hapo ndipo mshukiwa alimshawishi kijana huyo na kumvua nguo huku akimshika bila ruhusa yake na kumlazimisha kufanya mapenzi naye.

Kijana huyu aliokolewa na majirani ambao walipiga kamsa na kuwaita watu ambao walikusanyika na kumfumania peupe akila uroda na kijana huyo kinyume na sheria.

Akizungumza na wanahabari, bw. Makoma alisema kuwa vitendo kama hivi vimeongezeka katika maeneo ya Migori na Awendo.

Alitoa onyo kwa wakaazi wa eneo hilo kuwa makini na kupiga ripoti kwa polisi ama idara husika ili hatua za kisheria zichukuliwe kwa watu kama hao.

Aidha bw. makoma alitoa mwito kwa wakaazi wa eneo hilo kuheshimu maslahi ya vijana na watoto hasa wa shule ili kujenga maisha yao ya siku za usoni.

No comments:

Post a Comment