Wednesday, 3 October 2012

Mwanamke afungwa miaka matatu kwa kumwiba mtoto wa miaka miwili

24 SEPTEMBA, 2012

NA MONICA OKWANY

Mwanamke mwenye umri wa makamo amepewa kifungo cha miaka mitatu baada ya kuiba mototo wa miaka miwili.

 Irene Ayambuta alitekeleza wizi huo mnamo tarehe 18/9/2012 katika mtaa wa Oruba, kaunti ya Migori.

 Bi Grace Wanyenyi Mutatiro alimwacha mwanawe Faith Wati akicheza na wenzake na kwenda sokoni kulangua parachichi na aliporudi alimkuta mtoto wake hayupo.

 Aliambiwa na majirani kwamba mtoto wake alikuwa amechukuliwa na mwanamke ambaye hawakumtambua. Alimtafuta mtoto wake hadi nchi jirani ya Tanzania.
 
Alipata habari siku mbili baadaye kwamba mtoto wake alipatikana. Hapo ndipo wananchi walimvamia Bi Irene na kumpiga na kumjeruhi vibaya.

Aliokolewa na polisi ambao walimpeleka katika hospitali ya wilaya ya Migori kwa matibabu kabla ya kupelekwa korokoroni.

Alikubali mashtaka mbele ya hakimu mkaazi Bw. Edwin Nyaga ambaye alimpa kifungo cha miaka mitatu.

No comments:

Post a Comment