Wednesday, 3 October 2012

Mvuvi afariki Migingo

Wavuvi katika kisiwa cha Migingo. Picha na Monica Okwany
TAREHE 21 SEPTEMBA

NA MONICA OKWANY.

Mwanamme mvuvi aliye na umri wa miaka 36 alizama katika kisiwa cha Migingo katika Ziwa Victoria kaunti ya Migori.

Mvuvi huyo anayetambulika kama Erick Ochieng Ouma alikumbana na kifo chake wakati akienda haja ndogo

Wenzake waliokuwa naye wamesema kwamba wakati marehemu alikuwa akienda haja ndogo, mawimbi makubwa yalizuka na kufanya mashua yao kutikisika hali iliyomfanya kuanguka majini.

Juhudi za kumsaka hazikufua dafu kwani mawimbi yalikuwa makali nayo giza nene ilikuwa imetanda.

Akithibitisha kisa hicho, mkuu wa polisi mjini Nyatike Bw Richard Bitonga alisema kwamba marehemu aliteleza kutoka kwa mashua waliokuwa wakitumia na wenzake watatu, na kuanguka ziwani.

Bw. Bitonga alitoa tahadhari kwa wavuvi katika eneo hilo kuwa makini katika shughuli zao na vilevile kuepuka matumizi ya madawa za kulevya wakati wakiwa baharini.

No comments:

Post a Comment