Wednesday, 3 October 2012

Wanafunzi wajeruhiwa baada ya ukuta wa shule kuporomoka

19/09/2012
NA MONICA OKWANY

Wanafunzi wanne wa shule ya msingi ya Pesoda wajeruhiwa baada ya ukuta unaozingira shule hiyo kuporomoka na kuwaangukia.

Akithibitisha kisa hicho mwalimu mkuu wa shule hiyo Bw Issac Maeri alisema kwamba ajali hiyo ilitokea mnamo saa 3.40 jioni wakati wanafunzi walikuwa michezoni.

Majeruhi walipelekwa katika hospitali jirani ya Oruba Nursing Home kwa huduma ya kwanza kabla ya kupelekwa katika hospitali ya misheni ya Ombo.

Kati ya wanafunzi walioumia ni wavulana wanne, watatu wakiwa katika darasa la tano na mmoja katika darasa la kwanza.

Wawili waliopata majeruhi madogo madogo walichukuliwa na wazazi wao na kupelekwa hospitalini kwa matibabu.

Mmoja alipata majeraha kichwani na mwingine mguuni .Wawili hao bado wako hospitalini lakini hali yao inaimarika .

Ajali hiyo ilisababishwa na shimo iliyokuwa ikichimbwa na hospitali ya ‘oruba nursing and maternty home’ kando ya ukuta wa shule hiyo.

No comments:

Post a Comment